24.2 C
Dar es Salaam
Monday, May 6, 2024

Contact us: [email protected]

Umsota kuongeza wanachama

Na Victoria Godfrey, Dar es Salaam

Umoja wa Wachezaji soka wa zamani Tanzania (UMSOTA) una mpango wa kuhamasisha wachezaji wa zamani kujiunga kwenye umoja huo.

Akizungumza na www.mtanzania.co.tz Mwenyekiti wa UMSOTA,nFaza Lusozi, amesema tayari wameunda timu ya uhamasishaji ambayo itashirikisha magwiji wa mpira.

Amesema sasa wapo kwenye mchakato waliopata viwanja vya kufanyika mazoezi ili kuanza jukumu la uhamasishaji ambalo litaanza Dar Es Salaam na kufuatiwa mikoa mingine .

Mwenyekiti huyo amesema kuwa mpango huo itafanyika kwa mzunguko ili kuongeza idadi kubwa ya wanachama.

“Maandalizi yameanza kwa kuunda timu ya uhamasishaji ambayo itakuwa na jukumu la kuhamasisha watu wajiunge katika chama chetu,” amesema Lusozi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles