24.7 C
Dar es Salaam
Tuesday, March 19, 2024

Contact us: [email protected]

‘Kilichokamatwa ni chenga za mkaa sio dawa za kulevya’ Kiboko

DAR ES SALAAM

MFANYABIASHARA Ayubu Kiboko amedai mahakamani kwamba kilichokamatwa nyumbani kwake ni chenga chenga za mkaa sio chenga zinazosadikiwa kuwa dawa za kulevya.

Kiboko ameiomba Mahakama Kuu Kitengo cha Rushwa na Uhujumu Uchumi imwachie huru na amekana tuhuma kujihusisha na biashara haramu ya dawa.

Kiboko amedai hayo leo wakati akijitetea kwa kuongozwa na Wakili Majura Magafu mbele ya Jaji Lilian Mashaka.

Kibiko alikana vielelezo vivyotolewa na upande wa Jamhuri ambavyo ni chenga au unga uliokuwa katika mfuko wa nailoni angavu, vikopo viwili vyenye unga mweupe, mfuko mweusi wenye unga mweupe ndani na mfuko unaodaiwa kukutwa kwenye eneo la kutunzia viatu ambapo alidai kuwa vyote hivyo hakuwahi kuviona zaidi ya kuviona mahakamani na siku hiyo hakukufanyika upekuzi katika eneo la kutunzia viatu.
Kiboko amemaliza kujitetea bado mkewe Pili ambaye anatarajiwa kuanza utetezi wake.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
584,000SubscribersSubscribe

Latest Articles