24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

FILAMU YA DI CAPRIO, WINNIE MANDELA KUONYESHWA ZIFF

Na FESTO POLEA, DAR ES SALAAM


JULAI 8 hadi16, mwaka huu, wadau wa filamu kutoka nchi zaidi ya 70 watajumuika pamoja kushuhudia filamu zaidi ya 100 zitakazoonyeshwa kwenye Tamasha la 20 la Kimataifa la Filamu Zanzibar (ZIFF) kwenye Ukumbi wa Ngome Kongwe, visiwani Zanzibar.

Kati ya filamu hizo, ipo filamu ya makala ya prodyuza na mwigizaji maarufu kutoka Hollywood, Leonardo di Caprio inayoitwa ‘The Ivory Game’.

Filamu nyingine ya makala itakayoonyeshwa ni ya mwanaharakati Winnie Mandela kutoka Afrika Kusini iliyoongozwa na Pascale Lamche na nyingine ni ya Whitney Houston ya ‘Can I Be Me’ iliyotengenezwa na Nick Broomfield.

Mkurugenzi wa tamasha hilo, Fabrizio Colombo, alisema licha ya ugumu katika uchaguzi wa filamu unaotokana na ubora wa filamu walizopokea, wanaona umuhimu na mchango wa ZIFF katika maboresho ya filamu zilizowasilishwa kwao.

Colombo alisema watengeneza filamu kutoka nchi zaidi ya 70, wametuma filamu zao wakiwamo Tanzania, wengine ni Kenya, Canada, Hispania, Ufaransa, Afrika Kusini, Tanzania, India, Australia, Marekani, Nigeria, Rwanda, Brazil, Ghana, Chad, Uganda, Msumbiji, Hungary, Uingereza na Ethiopia.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles