24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

WAZIRI AWAACHIA NENO GUMU WAFANYABIASHARA WA MADINI

Na ELIYA MBONEA-ARUSHA


WAFANYABIASHARA wa madini (Dealers), wametakiwa kutembelea Gereza la Kisongo jijini hapa kusaidia wafungwa na mahabusu maji kwani hawajui nini kitafuata miongoni mwao.

Kauli hiyo ilitolewa jijini hapa hivi karibuni na Waziri wa Madini, Angela Kairuki, alipofanya mazungumzo ya kina na Chama cha Mawakala wa Madini Tanzania (TAMIDA).

Akizungumza na wanachama hao, Waziri Kairuki aliwataka kuanza kujitafakari upya kwa waliokuwa hawalipi kodi na kushiriki mbinu za utoroshaji madini kwani hawapo salama.

“Kabla ya kushiriki kutorosha madini jitafakari upya, unaipenda familia na wanaokutegemea? Ningeomba muanze kulitembelea Gereza la Kisongo kawasaidia maji wafungwa kwa sababu hamjui nini kitafuata kwenu.

“Ninasema haya si kwamba nawatisha, napenda sana muwe na mafanikio katika biashara hii, lakini kwa kufuata sheria na taratibu za nchi. Haitapendeza siku moja unajikuta umepata kosa la uhujumu uchumi.

“Siwatishi, mimi ni mama na dada yenu, ninawapa ushauri tusifike huko, tamaa ya muda mfupi itagharimu na kuleta athari kwa familia zenu na wanaowategemea,” alisema.

Aliwataka wafanyabiashara hao kuhakikisha wanafuata na kutekeleza kila kilichopo kwenye leseni zao, ikiwamo kusoma na kuzifanyia kazi sheria za madini.

“Tutaendelea kufanya marekebisho ya sheria ili ziwe kali zaidi. Niwaombe hakikisheni mnasafisha nyumba yenu na kuanzia sasa tukubali kubatizana upya na kufungua ukurasa mwingine,” alisema Waziri Kairuki.

Kwa upande wake, mwekezaji wa Kampuni ya Tanzania One inayofanya kazi kwa ubia na Serikali kupitia Shirika la Madini (Stamico), Faisal Juma, alisema watahakikisha taifa linanufaika na biashara wanayoifanya.

“Nikuhakikishie Mheshimiwa Waziri tupo tayari kufanya kazi na kuona taifa likinufaika. Tunajua wakati huu si wa kulumbana na Serikali,” alisema Juma.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles