23.6 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

WAMAREKANI WAMTAKA TRUMP ATANGAZE KODI ALIYOLIPA SERIKALINI

CALIFORNIA, MAREKANI


MAKUMI kwa maelfu ya watu katika miji mbalimbali nchini hapa wameendesha wakitaka Rais Donald Trump atangaze kodi aliyolipa kwa Serikali, jambo ambalo yeye binafsi amekataa kulifanya.

Waandamanaji wengine walibeba sanamu kubwa za kuku, wakimaanisha Rais ni mwoga na amekataa kutoa takwimu za kodi yake.

Karibu watu 14 wametiwa mbaroni huko Berkeley katika jimbo la California ambako wafuasi wa Rais Trump na wapinzani wake walikabiliana.

Ingawa hakuna sheria inayomlazimisha Trump kutangaza kodi yake, marais wote wa Marekani wamekuwa wakifanya hivyo kwa muda wa miongo minne iliyopita.

Maandamano hayo yalipangwa kwenda sambamba na siku ya mwisho ya raia kuwasilisha takwimu zao za kodi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles