30.2 C
Dar es Salaam
Friday, May 3, 2024

Contact us: [email protected]

TPHPA yatoa miche 60 ya matunda kwa shule nne Dar es Salaam

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

MAMLAKA ya Afya ya Mimea na Viuatilifu (TPHPA) Kanda ya Mashariki, imegawa miche ya matunda katika Shule za Sekondari za Diplomasia, Uhamiaji, Mwalimu Nyerere na Kiungani zilizopo jijini Dar es Salaam.

Akizungumza leo Juamosi Machi 9, 2024 kwa niaba ya Mkurugenzi Mkuu wa TPHPA, Profesa Joseph Ndunguru, Meneja wa Kanda ya Mashariki, Dk. Mahamudu Sasamalo alisema wamegawa jumla ya miche 60 ikiwa ni kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan za kutaka Watanzania watunze mazingira kwa kupanda miti.

“Sisi kama TPHPA tumeamua kutoa miti ya matunda na hasa mashuleni kwa kuhakikisha kuwa watoto wetu wanapata hewa safi, kivuli na zaidi wapate matunda,” amesema Dk. Sasamalo.

Amesema TPHPA inaendelea na jitihada za kutunza mazingira kwa vile afya ya binadamu na wanyama ni miongoni mwa jukumu lao.

“Lakini sote tuna wajibu wa kutunza mazingira na kupanda miti, ina faidi nyingi sana,” amesema Dk. Sasamo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles