RAPA Jayceon Terrell ‘The Game’, amemnunulia zawadi ya gari aina ya Ferrari msanii mwenzake, Sean Combs ‘P.Diddy’, baada ya kumkutanisha na prodyuza Dr. Dre.
Katika mtandao wa TMZ, Game alieleza kwamba haikuwa rahisi kufanya kazi na Dr Dre, lakini kupitia Diddy aliweza kufanikisha ndoto yake na mtayarishaji huyo kazi zilizompa mafanikio aliyonayo hivi sasa.
“Bila Diddy nisingepata dili la kurekodi na Dr, hivyo kama shukrani nimeamua kumpa zawadi hii ndogo ya gari, nimekumbuka tulipotoka kabla ya kuwa hapa nilipo nilikuwa karibu na Diddy sasa kwanini nisimshukuru kwa kuniunganisha na Dr Dre,” alisema The Game.