25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Staa filamu akutwa amefariki

MWIGIZAJI mwenye jina kubwa nchini Marekani, Michael K Williams, amekutwa amefariki dunia ndani ya nyumba yake jijini New York.

Kwa mujibu wa taarifa ambazo hazijathibitishwa na polisi, Williams aliyekuwa na umri wa miaka 54 aliiaga dunia baada ya kuzidiwa na kiwango kikubwa cha dawa za kulevya alizokuwa ametumia.

Ikumbukwe kuwa Williams aliyeng’ara vilivyo kwenye tamthilia ya ‘The Wire’, aliwahi kukiri kuteswa na utumizi wa dawa za kulevya. Juu ya kifo chake, polisi wa New York wamesema walifika nyumbani kwake jana na ni baada ya kupigiwa simu na watu wa karibu wa msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles