WAKAZI wa eneo linalokabiliwa na janga la ukame nchini India wametumia njia ya kuwatembeza utupu watoto wa kike kwa kile wanachoamini kitasaidia mvua kunyesha.
Katika tukio hilo lililotokea mjini Bundelkhand, watoto wa kike sita wenye umri mdogo wanaonekana wakiwa bila mavazi mbele ya umati, huku wakizunguka wakiwa wameshika fimbo zilizowekwa wadudu aina ya vyura.
Kwa mujibu wa imani za wakazi wa eneo hilo lililoko kwenye Jimbo la Madhya Pradesh, kitendo hicho kitamfurahisha mungu wa mvua na kuwaondolea balaa la ukame linalowatesa.
Aidha, Tume ya Kulinda Haki za Watoto ya India imelaani vikali, ingawa polisi wa eneo hilo wamesema hawajapokea taarifa rasmi juu ya kutokea kwa tukio hilo lakini wameanza uchunguzi.