24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Rufaa za kodi 1000 zalalamikiwa na wananchi

Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.
Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji.

NA FERDNANDA MBAMILA, DAR ES SALAAM.

MAMLAKA ya Mapato (TRA) na wadau wa kodi (TRA)  imesema imejipanga vizuri kuhakikisha kuna umakini zaidi katika kukadiria kodi ili kuepuka migogoro zaidi.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Dar es Salaam, Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dk. Ashatu Kijaji, alisema kwa kipindi cha mwaka 2001  hadi Agosti mwaka huu rufaa za kodi 1,354 zimewasilishwa  mbele ya  Baraza la  Rufaa ambapo  kati ya hizo ni kodi ya mapato.

“Wadau wa kodi hasa washauri wafanye kazi zao kwa weledi, hasa katika kuwashauri wafanyabiashara kutimiza wajibu wao ili kuondoa ubishi usiokuwa na msingi wa kulipa kodi na kuepuka kuathiri ubora wa maamuzi yanayotolewa na TRA,” alisema Dk. Ashatu.

Alisema  kuna ongezeko la thamani na ushuru wa forodha na rufaa zinajumuisha  jumla ya  kodi ya shilingi  trilioni 4 lakini  kutokana na hilo kuna kesi  ambazo kodi  yake  iko kwenye  dola milioni  443 kati ya rufaa  914 zilizonyimwa maamuzi.

“Mpaka sasa kuna  rufaa 440 ambazo bado ziko katika hatua mbalimbali za  usikilizwaji  kabla ya kufanyiwa maamuzi, na idadi hii ya kesi ni kubwa kulinganisha na wingi wa kesi ambazo zinazidi kuwasilishwa katika Baraza la  Rufaa kila mwaka,” alisema.

Alisema kwa mwaka  2013 na 2015 kulikuwa na kiwango cha pamoja  cha kodi ya Sh milioni 894 kilichobishaniwa  hadi kufikia Agosti mwaka huu.

“Kiwango hicho cha kodi  ambacho kipo  katika kesi  za mwaka huu peke yake ni shilingi trioni 2.4 na kutokana na takwimu hiyo, kiwango cha kodi kinacholalamikiwa hadi sasa kitazidi kuendelea kupanda mwaka hadi mwaka,” alisema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles