Katika ziara yake hiyo ya kwanza tangu dhoruba hiyo ilipotokea, Trump katika mazungumzo yake juu ya gharama ya kurejesha maisha upya amesema kwamba watawasaidia kupitia bajeti ya serikali yake.
Hata hivyo, wakaazi walio wengi bado wana hasira kwa serikali yao kwa namna wanavyoshughulikia suala hilo.
Zaidi ya asilimia tisini na nane ya watu hawana nishati ya umeme na walio wengi zaidi hawana maji safi na salama ya kunywa.