25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Polisi yanasa 9 kwa kulima bangi

bangiNa WALTER MGULUCHUMA –

SUMBAWANGA

 

Akizungumza na MTANZANIA jana, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, George Kyando, aliwataja watuhumiwa hao kuwa ni Pascha Ramadhani (48), Elisi Ulaya (45), Wilbeth Ramadhani na George Kapombe (43).

Wengine ni Radislaus Ntinda (33), Festus Misala (38), Cletus Kanyama (27), Lodrick Kanyama (56) na Flowin Misali (25). Watuhumiwa wanatarajia kupandishwa kizimbani baada ya upelelezi kukamilika.

Alisema pamoja na operesheni hiyo, ushirikiano mzuri kutoka kwa wananchi wema waliotoa taarifa umesaidia kukamatwa kwa watuhumiwa hao.

Alisema kilimo cha bangi kimeanza kujitokeza mkoani Rukwa, kitendo ambacho ni hatari na kuongeza kuwa iwapo jitihada za kukomesha hazitachukuliwa haraka, hali itakuwa mbaya.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles