23.6 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Kiwango cha elimu chamshtua RC

jordan-rugimbanaNa SARAH MOSES – DODOMA

KUTOKANA na kushuka kwa kiwango cha elimu mkoani Dodoma, Mkuu wa Mkoa wa Dodoma, Jordan Rugimbana,  ametoa siku 14 za kukutana na wakuu wa wilaya zote, wakurugenzi wote, maofisa elimu na viongozi wa Chama cha Walimu (CWT) ngazi zote, kufanya kikao cha pamoja ili kupata ufumbuzi wa kupandisha kiwango cha elimu mkoani hapa.

Agizo hilo alilitoa juzi, wakati akifungua warsha iliyoandaliwa na baraza la walimu kitengo cha wanawake kwa lengo la kujifunza mambo mbalimbali.

Pia amelitaka Baraza la Walimu Kitengo cha Wanawake Mkoa wa Dodoma kuhakikisha wanatafuta ufumbuzi wa kuboresha elimu kwa watoto wa kike, hususan wanaotokana na mazingira magumu na hatarishi.

Alisema ili kufanikisha sera ya elimu bure, lazima kiwango cha ufaulu kiongezeke shuleni, hususan katika Mkoa wa Dodoma.

Alisema hajafurahishwa na matokeo ya mkoa huo, kwa  kuwa nyuma kielimu, badala ya kushika nafasi nzuri yenye hadhi ya kuwa makao makuu.

“Sijapendezwa hata kidogo kuona Mkoa wa Dodoma unakuwa nyuma kielimu kutokana na hali ya sasa ya sera ya serikali ya elimu bure, lazima kuwapo na mikakati ya kukuza elimu kwa vijana wetu,” alisema Rugimbana.

Kwa upande wake, mwakilishi wa baraza hilo, Renatha Simbachawene, alisema kushuka kwa elimu ni changamoto ambazo zinasababishwa na wazazi kutokuwa karibu na walimu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles