29.2 C
Dar es Salaam
Thursday, May 9, 2024

Contact us: [email protected]

Milioni 250 zatengwa kwa vijana 20 wenye mawazo bunifu kuhusu matumizi ya nishati

Na Ramadhan Hassan, Dodoma

Jumla ya Sh milioni 250 zimetengwa kwa vijana 20 watakaoshinda wazo la ubunifu kuhusu changamoto ya ufanisi katika nishati nchini lengo likiwa ni kuimarisha mazingira ya matumizi bora kwa kukuza ubunifu na uvumbuzi.

Hayo yameelezwa leo Machi 15, 2024 jijini Dodoma na Afisa Mawasiliano kutoka Mpango wa Maendeleo wa Umoja wa Mataifa (UNDP), Jolson Masaki wakati akizungumza kwenye uzinduzi wa kutatua changamoto ya ubunifu kwa ufanisi wa nishati.

Mpango huo ni kwa kushirikiana kati ya Wizara ya Nishati, Umoja wa Ulaya (EU), Ubalozi wa Ireland na Shirika la Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

Masaki amesema Mpango huo unaungwa mkono na hazina kubwa ya Sh milioni 250 za Kitanzania na unafanywa ili kuimarisha mazingira ya matumizi bora ya nishati kwa kukuza ubunifu na uvumbuzi.

Amesema ruzuku hizo zinalenga kutoa usaidizi wa kifedha na kuwatia moyo wale wanaoonyesha uwezo wa kipekee katika kuunda mustakabali wenye ufanisi zaidi wa nishati kwa taifa.

Amesema wahitimu 20 waliochaguliwa watashiriki katika kambi ya mafunzo ya wiki moja ambapo watapokea mafunzo kutoka kwa wataalam wa nishati ili kuboresha mawazo/miradi yao.

Amesema mwisho wa maombi ni mwishoni mwa Aprili, mwaka huu.

“Kufuatia tukio hilo, wahitimu watashiriki katika programu ya ushauri kwa muda wote wa mradi. Kwa kuzingatia Mpango Kazi wa Ufanisi wa Nishati wa Tanzania, changamoto hii inajaribu kutumia werevu wa Wavumbuzi wa Kitanzania ili kukabiliana na changamoto kubwa ya ufanisi wa nishati,” amesema Masaki.

Vilevile, inalenga kuchochea maendeleo ya ufumbuzi wa busara ambao sio tu kupunguza matumizi ya nishati yasiyo endelevu lakini pia kuzingatia kanuni za uendelevu na utunzaji wa mazingira.

Kwa upande wake mtaalamu wa matumizi Bora ya Nishati, Robert Washija amewataka watanzania kuchangamkia fursa hiyo hasa vijana.

“Lengo ni kuhakikisha Tanzania inakuwa na matumizi bora ya Nishati.Tuna Vifaa vingi havina ubora hivyo kujikuta tukipoteza nishati nyingi,” amesema mtaalamu huyo.

Naye, Mwakilishi kutoka Wizara ya Nishati, Collins Lwanga amewataka watanzania kuchangamkia fursa hiyo ya wazo la ubunifu kuhusu matumizi bora ya nishati.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles