24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Matatu  yazuiwa kuingia katikati ya Nairobi

NAIROBI, Kenya



AGIZO la kuyazuia mabasi ya abiria kuingia katikati mwa mji mkuu   Nairobi lilianza kutekelezwa rasmi jana asubuhi na kusababisha adha kubwa kwa wasafiri baada ya polisi na mgambo kumwagwa katika njia kuu.

Hali hiyo ilisababisha   misululu mirefu ya abiria ambao walikuwa wakishushwa mbali na mji hususan barabara ya Thika wakitembea kwa  miguu kuelekea maeneo mbalimbali ya mji huu.

Katika agizo hilo, waendesha mabasi hayo maarufu kama  matatu, wameagizwa kuendesha shughuli zao  katika maeneo ambayo yametengwa bila kuingia katikati ya mji kuchukua ama kususha abiria.

Maofisa wa jiji wanasema   wamekwisha kutenga maeneo maalum yenye maegesho  505  yanayoweza kutumika kwa kazi hiyo.

Hata hivyo waendesha mabasi hayo ya abiria wanaomba kupewa muda zaidi kujiandaa   huku wakitishia kutafuta msaada wa  sheria kama mamlaka husika hazitasikiliza kilio chao na kusimamisha kwa muda agizo hilo.

Katika malalamiko yao, waendesha mabasi hao wanadai  wanahofia hali inaweza kuwa mbaya  mvua itakapoanza kunyesha ikizingatiwa maeneo waliyotengewa kutokuwa na vibanda vya kujikinga mvua.

Kwa mujibu wa taarifa zilizopatikana mjini hapa, agizo hilo ni mpango wa serikali wa kujaribu kuzuia msongamano wa magari katikati ya jiji hili.

Taarifa hizo zilieleza kwamba jana, zaidi ya  maofisa 300,  walipewa jukumu hilo  kuhakikisha agizo hilo linatekelezwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles