KIUNGO wa zamani wa Simba SC, James Kotei, amesajiliwa na Sohar ya Ligi Kuu ya Oman akiwa mchezaji huru.
Kotei raia wa Ghana, aliondoka Simba mwaka juzi na kutua Kaizer Chiefs lakini aliachwa na kisha kunaswa na Slavia Mozyr ya Belarus iliyotemana naye mwaka jana.
Itakumbukwa kuwa Kotei aliachwa na Kaizer akiwa hajacheza hata mechi moja ya ushindani.