23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Johanna amshinda Venus na kutwaa ubingwa WTA

Johanna Konta
Johanna Konta

CALIFORNIA, MAREKANI

NYOTA wa mchezo wa tenisi raia wa nchini Australia, Johanna Konta, ametwaa ubingwa wa michuano ya WTA baada ya kumshinda bingwa mara saba wa Grand Slam, Venus Williams.

Venus amejikuta akiwa katika wakati mgumu kwa mara ya pili, ikiwa ni wiki mbili zilizopita akitolewa kwenye nusu fainali ya michuano ya Wembledon, huku mdogo wake, Serena Williams, akitwaa ubingwa huo.

Katika mchezo wa juzi, Konta mwenye umri wa miaka 25, alifanikiwa kumshinda bingwa huyo mwenye umri wa miaka 36, kwa seti 7-5 5-7 6-2.

Hata hivyo, mshindi huyo amedai kwamba furaha yake kubwa ni kuweza kushinda mbele ya bingwa wa mchezo huo, hivyo atakuwa na furaha ya muda mrefu.

“Furaha yangu ni kufanikiwa kutwaa ubingwa huu mbele ya nyota wa mchezo huu, najua haikuwa kazi rahisi kushinda taji hili kwa kuwa mpinzani wangu anajulikana kwa kuwa na uwezo mkubwa.

“Nilikuwa na wasiwasi mkubwa baada ya kugundua kuwa nitacheza na Venus, lakini uwezo wangu umenifanya niwe hapa kwa sasa, mpinzani wangu ana uzoefu mkubwa na ametwaa mataji mengi ila kwa upande wangu ninaamini nimefanya vizuri zaidi,” alisema Johanna.

Kwa upande wa Venus naye amempa pongezi mpinzani wake Johanna kwa ushindi huo ambao ameupata na amemtaka kujituma zaidi ili kuweza kufanya vizuri katika michuano mingine.

“Johanna alistahili kushinda, alionesha uwezo wa hali ya juu japokuwa nilimpa changamoto mbalimbali, ninaamini ataendelea kufanya vizuri katika michuano mingine kutokana na uwezo wake ambao anauonesha.

“Kikubwa anatakiwa kupambana kwa kufanya mazoezi ya nguvu ili kujihakikishia anafanya makubwa zaidi katika michuano mingine,” alisema Venus.

Hata hivyo, mchezaji huyo anadaiwa kufanya vizuri tangu Januari mwaka huu ambapo aliweza kufika kwenye fainali ya michuano ya wazi ya Australia na michuano ya Eastbourne, Juni mwaka huu.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles