27.6 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Halotel yatoa msaada wa Chakula na vifaa vya nyumbani kwa Wanawake wenye mahitaji maalumu Mtwara

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Katika kuhadhimisha mwezi wa kumsheherekea Mwanamke na kukaribisha sikuukuu za Pasaka, Halotel Tanzania yatoa msaada kwa wanawake chini ya Taasisi ya ‘Jukwaa la wanawake na wasichana wenye ulemavu Mtwara’ kusaidia changamoto mbalimbali wanazozipata wanawkae hao.

Halotel ikiwa ni kampuni ya mawasiliano Tanzania, ikitoa huduma mbalimbali za mawasiliano na ikiendelea kukidhi mahitaji ya wateja wao. Kwa kuzingatia usalama na uaminifu Halotel inaendelea kutoa huduma bora na kuleta mabadiliko chanya katika sekta ya mawasiliano na jamii kiujumla.

Akiongea katika tukio hilo Mkurugenzi wa Halotel tawi la Mtwara, Emmanuel Monyo: “Halotel inaendelea kusimama imara katika kufanikisha malengo yake ya kukuza usawa na ujumuishaji katika pande zote za jamii. Lakini kwa kuwasaidia wanawake hawa Mtwara Halotel inaonyesha dhamira yake ya kuleta mabadiliko katika jamii na kuunda ulimwengu weye uwezekano na fursa kwa wote,”.

Halotel wakikabidhi msaada wa Vifaa vya nyumbani na Chakula katika taasisi ya Jukwaa la Wanawake walemavu Mtwara. Kushoto akiwa Mkurugenzi wa Tawi la Halotel Mtwara, Emmanuel Monyo, Kati ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Jukwaa la Wanawake walemavu Mtwara, Fatuma Mohamed Mkondomoka, Kulia Afisa uhusiano na Mawasiliano makao makuu Halotel Roxana Kadio.

Afisa uhusiano na mawasiliano wa Halotel, Roxana Kadio ambae aliwasilisha msaada huo alisema Halotel inaedelea kujenga ujumuishaji ambao kila mtu bila kujali uwezo wao anaweza kushiriki kikamilifu katika jamii, aliendelea kusema kuwa Halotel iliamua kuwasaidia wanawake wa Mtwara baada ya kujifunza kuwa wanapitia changamoto za chakula na vifaa vya nyumbani na kama kampuni inayokua nia yetu kutoa mkono wa msaada kwa jamii ya kitanzania.

 “Mahitaji yaliyotolewa na Halotel ni pamoja na Chakula kama Mchele, Sukari na Mafuta ya kupikia lakini pia kutoa msaada wa magodoro na vifaa vingine vya nyumbani. Vyote hivi ni katika kuwahudumia wanawake hawa na kuwaonesha kuwa hawako peke yao katika changamoto wanazozipita,” amesema Roxana

Ameongeza kuwa msaada huu pia unalenga katika kuwatoa upweke wanawake hawa katika mahitaji yao. Na kwamba Halotel haitoishia kusaidia tu wanawake na wako kwenye mpango wa kukuza uhitaji wa jamii kiujumla.

Halotel wakikabidhi msaada wa Vifaa vya nyumbani na Chakula katika taasisi ya Jukwaa la Wanawake walemavu Mtwara. Kushoto akiwa Mkurugenzi wa Tawi la Halotel Mtwara, Emmanuel Monyo, Kati ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Jukwaa la Wanawake walemavu Mtwara, Fatuma Mohamed Mkondomoka, Kulia Afisa uhusiano na Mawasiliano makao makuu Halotel Roxana Kadio.

Halotel itaendelea kutoa ushirikiano kwa majukwaa ambayo yanajikita katika kuwainua wanawake. Lakini pia Halotel itaendelea kutia chachu ya maendeleo kwa wateja wake na  jamii kiujumla.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles