23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Griezmann akatwa mshahara

MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Ufaransa, Antoine Griezmann, alilazimika kukata sehemu ya mshahara wake ili arudi Atletico Madrid.

Kwa mujibu wa taarifa, Griezmann amepunguza asilimia 40 ya mshahara aliokuwa akilipwa na Barcelona.

Griezmann alijizolea umaarufu mkubwa wa upachikaji mabao akiwa Atletico lakini alijikuta kwenye wakati mgumu alipohamia Barca mwaka juzi.

Kilichomfanya ashindwe kuwika Camp Nou na kufunga mabao 35 pekee katika mechi 102 ni mfumo uliomlazimisha kutocheza mshambuliaji wa kati ili kumpisha Lionel Messi aliyekuwa hatari kwenye eneo hilo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles