23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Davido ashangazwa na Chioma

LAGOS, NIGERIA 

STAA wa muziki nchini Nigeria, David Adeleke, maarufu kwa jina la Davido, ameshangazwa na mpenzi wake Chioma Rowland kuwa na uwezo mkubwa wa kuchora picha.

Davido alitumia ukurasa wake wa Instagram na kuposti picha ambayo imechorwa na mrembo na kisha kumpa kama zawadi.

“Mke wangu amechora picha hii na kunipa zawadi, asante sana mpenzi wangu, sikuwa nawaza kama angeweza kufanya kitu kikubwa kama hiki, naweza kusema ana kipaji cha hali ya juu, amenishangaza kwa kweli,” aliandika msanii huyo.

Miezi kadhaa iliyopita kulikuwa na taarifa kwamba wawili hao wapo kwenye mipango ya kufunga ndoa mwaka huu, lakini kutokana na janga la corona mipango hiyo inashindwa kukaa sawa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles