NEW YORK, MAREKANI
MWANAMITINDO maarufu nchini Marekani, Amber Rose, amefunguka na kusema yupo kwenye mipango ya kutaka kuolewa na rapa Shayaa Joseph anayejulikana kwa jina la 21 Savage.
Amber mwenye umri wa miaka 33, amesema mipango hiyo ya kutaka kuolewa na msanii huyo mwenye umri wa miaka 24 inaendelea kufanyika na tarehe rasmi itatangazwa.
“Nadhani sasa nipo sehemu sahihi kwa 21 Savage, ananifanya niwasahau wanaume wengine katika maisha yangu, siwezi kumsahau Wizkhalifa kwa kuwa ni baba wa mwanangu, lakini siwezi kumwelezea chochote kwa sasa.
“Kitu ambacho naweza kukizungumzia ni juu ya uhusiano wangu na 21 Savage, kilichopo kwa sasa ni juu ya kuja kuoana, nadhani kila kitu kitawekwa wazi kwa kuwa mambo ni mazuri,” alisema Amber.