MADRID, Hispania
MKUU wa benchi la ufundi la Real Madrid, Carlo Ancelotti, amesisitiza kuwa kikosi chake kina nafasi ya kutwaa taji la msimu huu wa Ligi ya Mabingwa Ulaya.
Madrid walikaribia kuishia hatua ya makundi kwenye michuano hiyo, kabla ya kuingia 16 bora kwa kuitandika Inter Milan mabao 2-0 usiku wa Jumanne ya wiki hii.
Licha ya hiyo, jeuri ya Ancelotti inatokana na kasi ya Madrid kwa siku za hivi karibuni, ambapo imeshinda mechi zote tisa zilizopita.
“Tuna ubora wa kutwaa La Liga na Ligi ya Mabingwa…” alisema kocha huyo akiongeza kuwa anafahamu udhaifu wa kikosi chake kwenye eneo la ulinzi.