PARIS, Ufaransa
MKURUGENZI wa michezo wa klabu ya Lyon, Juninho, ametangaza kuwa ataachia ngazi ifikapo Januari, mwakani.
Kama itakumbukwa, Mbrazil huyo aliyewahi kuichezea kwa mafanikio timu hiyo, ameshikilia wadhifa huo kwa miaka miwili na nusu.
Kwa upande wake, uongozi wa klabu hiyo haujazungumza chochote juu ya taarifa hiyo ya Juninho kusema atajiuzulu.
Ikiwa atandoka, ni wazi Lyon italazimika kuingia sokoni kumtafuta mtu wa kushika nafasi hiyo kwa kuwa ni muhimu kwenye uendeshaji wa soka la kisasa.