27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

New Zealand kupiga marufuku uvutaji sigara

WELLINGTON, New Zealand

NEW Zealand itapiga marufuku uuzaji wa tumbaku, lengo likiwa ni kukiondoshea kizazi kijacho utamaduni wa kuvuta sigara.

Katika sheria inayotarajiwa kuanza kufanya kazi mwakani, mtu aliyezaliwa baada ya mwaka 2008 hataruhusiwa kununua sigara au tumbaku kwa kipindi chote cha maisha yake.

“Tunataka kuhakikisha vijana hawaanzi kuvuta sigara,” amesema Waziri wa Afya, Dk. Ayesha Verall.

Wakati huo huo, madaktari na wataalamu wengine wa afya wameipongeza hatua hiyo. “Itasaidia watu kuacha (kuvuta) au kuhamia kwenye vilevi vingine visivyo hatari zaidi…” amesema Prof. Janet Hook, mhadhiri wa Chuo Kikuu cha Otago.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles