26.9 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

China: Waliosusia Olimpiki watakiona cha moto

BEIJING, China

SERIKALI ya China imezionya nchi zilizogoma kushiriki michuano ya Olimpiki ya mwakani itakayofanyika Beijing, ikisema zitajutia hatua yao hiyo.

Marekani, Uingereza, Australia na Canada hazitapeleka wanamichezo wake, huku sababu ikiwa ni janga la Corona na kufikisha ujumbe wa kulaani vitendo vya uvunjifu wa haki za binadamu nchini China.

Ikizungumzia hulo, China kupitia kwa Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje, imesema: “Marekani, Uingereza na Australia zimetumia Olimpiki kama jukwaa la siasa.”

Kwa upande wake, Ufaransa ambao ni wenyeji wa Olimpiki ijayo, wameweka wazi kuwa hawataungana na mataifa yatakayogomea mashindano hayo ya Beijing yanayotarajiwa kufanyika Februari.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles