LONDON, England
IMEBAINIKA kuwa Uingereza imeifanya Romania kuwa dampo kwa kutupa takataka zake kwenye nchi hiyo ya Kusini-Mashariki mwa Bara la Ulaya.
Ni katika uchunguzi wa Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), ndipo ilipofichuliwa kuwa takataka zinazozalishwa Uingereza husafirishwa na kwenda kutupwa Romania.
Mamlaka za Romania zimekiri hilo zikisema takataka hizo huingia kwa meli zikiitwa ‘bidhaa zilizotumika’ na zimekuwa na faida kwao, hasa katika kujaza ardhi zenye mabonde.
Kwa Uingereza, hapo imeisaidia kupunguza gharama kubwa ambayo wangeitumia kuweka mazingira mazuri ya kuzihifadhi takataka hizo nchini kwao.