Madrid, Hispania
Real Madrid wamepanga kumwajiri aliyekuwa mkurugenzi wa michezo wa Lille ya Ufaransa, Luis Campos.
Campos atapewa jukumu la kusimamia usajili wa majira ya kiangazi baada ya Madrid kuvurunda msimu huu uliomalizika.
Itakumbukwa kuwa Campos aliachia ngazi Lille mapema mwaka huu baada ya klabu hiyo kupata wamiliki wapya.
Mtaalamu huyo mwenye umri wa miaka 56, atakuwa na kibarua cha kuhakikisha anawanasa Kylian Mbappe na Erling Braut Haaland wanaofukuziwa na Madrid.