London, Uingereza
Hatimaye Chama cha Soka England (FA) kimemfutia adhabu ya kukosa mechi tatu za msimu ujao wa Ligi Kuu nahodha wa Chelsea, Cesar Azpilicueta.
Azpilicueta alishukiwa na rungu hilo baada ya kulimwa kadi nyekundu katika mchezo wa hivi karibuni dhidi ya Aston Villa, ambao Blues walishinda mabao 2-1.
Katika mechi hiyo ya mwisho kwa msimu huu, nyota huyo alipewa ‘umeme’ kwa kile mwamuzi alichokiona kuwa ni kumchezea rafu kiungo wa Villa, Jack Grealish.
Chelsea watashuka dimbani Jumamosi ya wiki hii kumenyana na Manchester City katika mtanange wa fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.