25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

WASHIKILIWA NA POLISI KWA MAUAJI

Na Pendo Fundisha, Mbeya

Jeshi la polisi Mkoa wa Mbeya, limefanikiwa kukamata silaha mbili ikiwemo Short Gun iliyokuwa ikimilikiwa na Kampuni ya Ulinzi ya Suma JKT, Itende mkoani humo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya, Mohammed Mpinga amesema haya leo wakati akizungumza na waandishi wa habari na kuongeza kuwa katika tukio hilo watu watano wanashikiliwa kwa kukutwa na silaha hiyo pamoja na mauaji ya Mlinzi wa Kampuni ya Ulinzi ya Suma JKT, Chewe Willison yaliyotokea Februari 26, mwaka huu.

Kamanda Mpinga, amewataja watuhumiwa hao kuwa ni Hamid Shaban, Ibrahimu Mbilinyi, Stany Wema, Bahati Layland na Sambas Samson.

Aidha, amesema watuhumiwa hao walipohojiwa na askari wamesema silaha hiyo waliagizwa na mtu ambaye jina lake limehifadhiwa kwa ‘dau’ la milioni tatu na kwamba anatafutwa na Polisi.

 

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles