23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Urusi yaadhimisha miaka mitano tangu iiteke Crimea

MOSCOW, URUSI

URUSI imeadhimisha mwaka wa tano tangu ilipoliteka jimbo la Crimea lillilokuwa sehemu ya Ukraine katika sherehe zilzoongozwa na Rais Vladimir Putin jana.

Rais Putin aliwasili jimboni humo na kuhudhuria maadhimisho hayo kwenye mji mkuu wa jimbo hilo, Sevastopol.

Hatua hiyo ya Urusi ya kuliteka jimbo la Crimea mwaka 2014 ililaaniwa vikali na Ukraine na nchi za magharibi lakini ilipongezwa na Warusi wengi.

Ikulu ya Urusi imesema katika taarifa kuwa kilichotokea  miaka mitano iliyopita ni kujiunga tena kwa rasi  ya Crimea na Urusi.

Rais Putin jana alifungua kituo kikubwa kipya cha nishati pamoja na kukutana na wanaharakati wa asasi za kiraia.
Awali miaka mitano iliyopita Rais huyo alitia saini mkataba na wawakilishi wa Crimea ili kuhalalisha jimbo hilo kuwa sehemu ya Urusi, muda mfupi tu baada ya kufanyika kura ya maoni ambayo haikutambuliwa na jumuiya ya kimataifa.

Waziri wa Mambo ya nje wa Ukraine, Pavlo Klimkin amesema miaka yote mitano imejenga mazingira ya ugaidi dhidi ya watu wa Crimea.

Lakini pia utafiti uliofanywa mapema mwezi huu umebainisha kuwa ni asilimia 39 tu ya Warusi wanaoamini Crimea imeleta manufaa kwa Urusi.

Mwaka 2014 Warusi waliounga mkono uvamizi huo  walikuwa asilimia 67 wakisema kutekwa kwa Crimea kulileta manufaa zaidi  kuliko hasara kwa Urusi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles