24.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Mbowe asikitishwa Lowassa kuondoka Chadema

Elizabeth Joachim, Dar es salaam

Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe, amesikitishwa na kitendo cha kuondoka kwa Waziri Mkuu mstaafu, Edward Lowassa kurudi katika Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo Ijumaa Machi 15, Mbowe amesema walimpokea Lowassa mwaka 2015 kwa nia njema lakini leo kaamua kurudi CCM.

“Kwenda kwenye chama kingine cha siasa siyo mbaya, basi akaseme kweli na akisaidie chama hicho kisiendelee kuwatesa Watanzania na sisi tutaendelea kuijenga demokrasia.

“Enzi za uhai wake Baba wa Taifa, Mwalimu Julius Nyerere, aliwahi kusema chama cha siasa ni dodoki ukiliweka kwenye maji litanyonya maji na ukiliweka kwenye maziwa litanyonya maziwa kilichobaki ni kujenga chama kwa kuongeza wanachama,” amesema Mbowe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles