23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

HUDDAH AMWONYESHA ‘SPONSA’  WAKE

NAIROBI, KENYA

MASHABIKI nchini Kenya walikuwa na maswali mengi juu ya safari za mrembo nyota nchini humo Huddah Monroe, lakini mrembo huyo ameamua kumwanika ‘sponsa’ wake wa kizungu anayesimamia bata zote.

Wiki iliopita mrembo huyo alikuwa mjini Monaco, mji ambao unatajwa kuwa wa gharama duniani na alionekana akiwa sehemu mbalimbali za starehe na kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliamua kumwanika sponsa huyo ambaye ni babu wa kizungu.

“Niliweka wazi kukaa mbali na mitandao ya kijamii, hii ni kutokana na mtu ambaye niko naye kwa sasa nipo na mzungu wangu nadhani hakuna maswali tena, baada ya hapa nahitaji niwe na babu mwingine nitafutieni,” aliandika Huddah.

Mrembo huyo alitumia ukurasa huo kuweka picha mbalimbali huku kwa mbali akionekana mzungu huyo amekaa pembeni, hivyo yalikuwa majibu kwa wale waliokuwa wanajiuliza safari za mrembo kwenda kura bata nje ya bara la Afrika zilifadhiliwa na nani.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles