31.2 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Yanga kufanya Birthday Mbeya

Na Winfrida Mtoi, Mtanzania Digital

Klabu ya Yanga imepanga kufanya sherehe ya kuadhimisha miaka 89 tangu kuzaliwa kwake Februari 11, 2024, jijini Mbeya siku ambayo itakutana na Tanzania Prisons katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 5, 2024 jijini Dar es Salaam, Ofisa Habari wa klabu hiyo, Ally Kamwe amesema tayari matukio mbalimbali kuelekea kilele cha maadhimisho hayo yameanza na kesho wanatarajia kuingia mkataba na hospitali kubwa nchini.

Amesema lengo la kuingia mkataba na hospitali hiyo ambayo hakuitaja jina ni kuweza kuwasaidia mashabiki wao katika suala la afya.

“Kesho Yanga inakwenda kusaini mkataba na hospitali kubwa sana duniani, ikiwa na lengo la kumnufaisha shabiki wetu kwenye masuala yanayohusu afya yao. Pia Jumatano tunazindua upya ofisi yetu pale Jangwani.

“Mkoa wa Mbeya umepata bahati ya kusheherekea ‘anniversary’ ya mabingwa wa kihistoria. Naomba mashabiki wote wa Yanga popote walipo wakaweke kambi Mbeya na tutazindua na nyimbo mbili kutoka kwa wasanii wakubwa,” amesema Kamwe.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles