24.8 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

WEMA SEPETU: NISAMEHENI NIPO KWENYE IBADA

Na KYALAA SEHEYE


MWIGIZAJI wa filamu za Bongo, Wema Sepetu, amewaomba radhi watu wote aliowahi kuwakosea na amesema amewasamehe wote waliomkosea.

Wema alisema kwa sasa ameelekeza ibada yake mwezi huu mtukufu wa Ramadhani ili kusudio alilojiwekea kabla ya mfungo huu litimie.

“Ninaamini kabisa ibada yangu ninayoifanya hadi usiku itapokelewa vyema na itafanikisha azma yangu na kuondoa makandokando na majina yote ya ajabu wanayoniita wasionitakia mema,” alisema Wema.

Wema aliongeza kwamba pia amechoshwa na tabia za watu wanaomhisia vitu vya ajabu ambavyo hajavifanya, vitu ambavyo hakuwa tayari kuvitaja huku akisisitiza kwamba imani yake kubwa kipindi hiki cha mfungo na ibada anazofanya zitawafedhehesha wenye nia mbaya naye.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles