25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Watu zaidi ya 57 wafariki dunia baada ya lori la mafuta kulipuka

Anna Potinus

Lori lililokuwa limebeba mafuta aina ya petroli likitokea Dar es Salaam limepinduka na kuwaka moto katika eneo la Msamvu mkoani Morogoro leo Jumamosi Agosti 10, ambapo takribani watu 57 wamepoteza maisha.

Akithibitisha kutokea kwa ajali hiyo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro, Wilbroad Mutafungwa, amesema walipokea taarifa ya kuanguka kwa gari iliyokuwa ikitokea Dar es Salaam lakini uelekeo wake haukufahamika ambalo lilianguka upande wa kushoto wa barabara likielekea uelekeo wa Dodoma, Iringa na baada ya kupinduka mafuta yalianza kumwagika.

“Watu wanaofanya shughuli katika eneo hili walianza kumiminika kwaajili ya kuchota mafuta ambayo yalikuwa yanamiminika kwa kasi kubwa lakini gafla ukajitokeza moto mkubwa ambao umesababisha watu takribani 57 kupoteza maisha lakini bado tunaendelea kufuatilia idadi kamili na miili hiyo kwa sasa iko hospitali huku ufuatiliaji ukiendelea ili kuwabaini majina yao,” amesema.

“Pia katika eneo hili tumekuta pikipiki zaidi ya 10 zikiwa zimeungua vibaya, bado tunafanya uchunguzi kujua zilikuja kufanya nini katika eneo hili tunadhani ni hao ambao walikuja kuchukua mafuta na zenyewe tunafanya utaratibu wa kuziondoka katika eneo hili,” amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles