24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Wananchi wajitokeza ufunguzi wa Wiki ya AZAKI Dodoma

Na Mwandisho Wetu, Dodoma

Wananchi mbalimbali wa Jiji la Dodoma wamejitokeza kwa wingi katika ufunguzi wa Wiki ya Asasi za Kiraia (AZAKI) ambapo mgeni rasmi alikuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai.

Maadhimisho hayo ya Wiki moja yaliyobeba Kaulimbiu ya ‘AZAKI NA MAENDELEO’ yalianza kwa matembezi maalum yaliyoanzia katika Shule ya Sekondari ya Dodoma na kuelekea katika viwanja vya ukumbi wa Jakaya Kikwete ambapo ndipo kulipofanyika shughuli za ufunguzi.

Washiriki wa Matembezi ya Wiki ya AZAKI wakiwa wameshika mabango yenye jumbe mbalimbali zinazohusu Asasi za Kiraia ikiwa ni siku ya kwanza ya Wiki ya Asasi za Kiraia iliyozinduliwa leo Jijini Dodoma. (PICHA NA HUGHES DUGILO)

Aidha, katika matembezi hayo yaliyofana sana washiriki walibeba mabango mbalimbali yenye jumbe tofauti za shuguli zinazofanywa na Mashirika ya Asasi za Kiraia ambazo zimekuwa na mchango mkubwa kwa Jamii ya watanzania na Taifa kwa ujumla.

Baadhi ya washiriki wa Matembezi hayo wamesema kuwa wameshiriki kwenye wiki ya Azaki mwaka huu kwaajili ya kuendelea kutoa elimu kwa jamii ili waweze kufahamu shughuli zao ambazo kimsingi zimejikita katika kuwasaidia kupaza sauti zao na kuibua changamoto katika jamii ili Serikali iweze kuzifanyiakazi, na kwamba wao kama Azaki wanaona kuwa ushiriki wao kwenye Wiki ya Azaki utawapa fursa ya kuendelea kukuza mashirikiano baina yao.

Askari wa Kikosi cha JKT Makutupora wakiongoza Matembezi katika uzinduzi wa Wiki ya Asasi za kiraia (AZAKI) matembezi ambayo yalianzia kwenye viwanja vya Shule ya Sekondari ya Dodoma saa tatu asubuhi.(PICHA NA HUGHES DUGILO).

Wiki ya AZAKI ni jukwaa pekee nchini linaloleta kwa Pamoja wadau wakuu wa maendeleo ikiwemo Serikali, Sekta binafsi na Asasi za Kiraia Pamoja na wananchi kwa lengo la kujadili masuala yanayohusu ustawi wa nchi na maendeleo ya Taifa kwa ujumla ambayo imezinduliwa rasmi leo Jumamosi Oktoba 23, na kufungwa Oktoba 28, 2021.

Baadhi ya Maafisa FCS wakishiriki matembezi maalum kuelekea kwenye uzinduzi rasmi wa Wiki ya Azaki iliyozinduliwa rasmi leo na Spika wa Bunge Mhe. Job Ndugai Jijini Dodoma. (wa kwaza kulia) ni Ayoub Masaki Meneja wa Fedha na uendeshaji wa FCS, (kua kwake) ni Karin Rupia Afasa wa FCS Uhamasishaji Rasilimali. (wa tatu kulia) ni Justice Rutenge mshauri wa Tathimini, na (wa pili kushoto) ni Afisa Mwandamizi wa Fedha wa FCS Maria Chang’a. (PICHA NA HUGHES DUGILO).
Mkurugenzi Mtendaji wa FCS Francis Kiwanga (katikati) akiwa na wadau wa Maendeleo Balozi wa Canada Nchini Tanzania Hellen Fytche (kulia) (PICHA NA HUGHES DUGILO).
- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles