24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Wakutwa na vipande 47 meno ya tembo

KULWA MZEE-DAR ES SALAAM

WAKAZI wawili wa Chanika Kwa Zoo, Dar es Salaam, wamefikishwa mahakamani kwa tuhuma za  kukutwa na vipande 47 vya meno ya tembo vyenye thamani ya zaidi ya Sh bilioni moja.

Washtakiwa hao, Abdallah Hamis (30) na Adam Kawàmbwa (35), walipanda kizimbani jana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu mbele ya Hakimu Mkazi, Augustino Rwezile.

Wakili wa Serikali, Candid Nasua alidai washtakiwa walitenda makosa hayo Februari 11, mwaka huu eneo la Chanika Kwa Zoo, Ilala Dar es Salaam.

Alidai kuwa katika shtaka la kwanza, washtakiwa hao walikutwa wakimiliki vipande 47 vya meno ya tembo vyenye thamani ya Sh 1,081,357,500 mali ya Serikali bila kibali kutoka kwa Mkurugenzi wa Wanyama Pori nchini.

Ilidaiwa kwamba katika shtaka la pili washtakiwa walitakatisha fedha hizo wakati wakijua zimetokana na kosa la ujangili.

Baada ya kusomewa mashtaka hayo, washtakiwa hawakutakiwa kujibu lolote kwakuwa mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza shauri hilo.

Wakili Nasua alidai upelelezi wa shauri hilo haujakamilika na kesi iliahirishwa hadi Machi 25, mwaka huu itakapotajwa.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles