23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

WAFUNGWA MAELFU WATOROKA GEREZANI DRC

ULINZI: Polisi wakituliza ghasia wakati wakilinda gereza lililovamiwa mjini Beni, DRC.

 

 

KINSHASA,   DRC

WAFUNGWA zaidi ya 900 wametoroka baada ya watu wenye silaha kuvamia  gereza moja mjini  Beni, DRC.

Kwa mujibu wa Gavana wa Mkoa wa Kivu Kaskazini, Julien Paluku,  uvamizi huo uliotokea juzi na washambuliaji hao walitumia silaha kali.

Watu 11 wameripotiwa kuuawa katika tukio hilo na bado waliofanya mashambulio hayo hawajajulikana.

Shambulio hilo  ni la nne kwa wafungwa kutoroka jela kutokea nchini humo ndani ya   mwezi mmoja uliopita.

Kwa mujibu wa polisi, wafungwa wapatao 4,000 walitoroka jela mwezi uliopita katika jela yenye ulinzi mkali katika mji mkuu wa Kinshasa ambako kundi la watu wanaopigania kujitenga lilihusishwa na hujuma hiyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles