24.8 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Wafanyabiashara waanza kuandaliwa bomba la gesi

ntalikwapsNa Veronica Romwald, Dar es Salaam

SERIKALI imeanza kuwaandaa wafanyabiashara wa ndani walioko kwenye sekta ya mafuta, jinsi watakavyoweza kuchangia na kunufaika na fursa mbalimbali zitakazojitokeza katika mradi wa bomba la mafuta ghafi.

Baadhi ya wafanyabiashara hao, leo wanaondoka nchni wamekwenda kukutana na Rais wa Uganda, Yoweli Museveni pamoja na wafanyabiashara wa mafuta wa nchi hiyo katika kikao kitakachojadili mradi huo.

Hatua hiyo, imechukuliwa baada ya Kenya kutaka mradi huo utakaogharimu Dola za Marekani bilioni nne ( zaidi ya Sh trilioni nane), unaotarajiwa kuanza mapema mwakani kutoka Tanga hadi nchini humo.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini, Profesa Justine Ntalikwa aliwaambia waandishi wa habari Dar es Salaam jana kuwa, Serikali imekutana na wafanyabiashara hao kwa kuwa Tanzania ina asilimia 98 ya kuupata mradi huo.

“Licha ya mvutano uliopo tumekutana na wafanyabishara zaidi ya 30, tumewaeleza fursa ambazo zitawanufaisha wao na nchi kwa ujumla ikiwamo kodi zitakazolipwa, kuongezeka kwa wigo wa ajira  na tenda mbalimbali zitakazotolewa wakati na baada ya kukamilika   ujenzi wa mradi huo,” alisema.

Alisema Tanzania ina kila sababu ya kupata mradi huo kwa kuwa ina uzoefu wa ujenzi wa mabomba mengine manne na inajivunia Bandari ya Tanga ambayo ina kina kirefu kuliko bandari zote Afrika Mashariki.

Akizungumzia mvutano uliopo na  Kenya kutaka mradi huo, Profesa Ntalikwa alisema mvutano huo ni suala la dplomasia, tayari mazungumzo kati ya Tanzania na Kenya yameanza kufanyika ili kuumaliza.

“Tunazungumza na Kenya kwa sababu wao ndiyo wenye ‘due deligence’… kama mnakumbuka mazungumzo ya awali juu ya ujenzi wa bomba hili yalikuwa kati ya Uganda na Kenya. Tanzania hatukushirikishwa walikubaliana kuunda kamati iliyohusisha wataalamu wa Kenya na Uganda.

“Kamati hiyo ya watalaam walipanga kutafuta data (takwimu) wapi patafaa kujengwa mradi huo, walipanga kuanzia kufuatilia data hizo kuanzia Lamu (Uganda), Mombasa (Kenya) hadi Tanga (Tanzania),” alisema.

Alisema kwa kuwa Tanzania haikushirikishwa katika makubalino hayo imepanga kupeleka ombi kwa serikali ya Uganda kwamba haitashiriki kukusanya data hizo huko Lamu badala yake itashiriki kuzitafuta za Tanga pekee.

Mwenyekiti wa Wafanyabiashara wa Sekta ya Mafuta Tanzania, Dk. Gideon Kaunda alisema wamejipanga kujitoa mhanga na kujidhatiti kuwekeza katika bishara kwenye mradi huo.

“Tunakwenda Uganda kumshawishi Museveni, tumejidhatiti na tumejitoa mhanga tutawaeleza kwa nini Tanzania inafaa kuwekeza mradi huo,” alisema.

Machi 2, mwaka huu, marais John Magufuli na Yoweri Museveni walikubaliana juu ya ujenzi wa bomba hilo litakalokuwa na urefu wa kilometa 1,120.

Mradi huo utatoa fursa za ajira kwa watu 15,000  utakapoanza lakini pia uwekezaji huo unalenga kuongeza pato la taifa na kukuza uchumi wa nchi hizo mbili.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles