25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

TIC yawashauri Watanzania kuwekeza nchini

Mkurugenzi wa Masuala ya Kitaasisi, Suleiman Mzava (kushoto) akizungumza na baadhi ya wateja waliofika kwenye banda lao kwa ajili ya kufahamu masuala mbalimbali yanayohusu uwekezaji.
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Pendo Gondwe akimueleza fursa za Uwekezaji zilizopo nchini, Waziri wa Katiba na Sheria, Dk. Damas Ndumbaro alipotembelea banda hilo katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam Julai, 2022.
Meneja Uhusiano na Mawasiliano wa Kituo cha Uwekezaji Tanzania (TIC), Pendo Gondwe akimueleza fursa za Uwekezaji zilizopo nchi nchini, Shaka Hamdu Shaka Katibu wa Itikadi na Uenezi Taifa wa Chama Cha Mapinduzi alipotembelea banda hilo katika maonesho ya Sabasaba yanayoendelea jijini Dar es Salaam, Julai, 2022.

Na Hadia Khamis, Mtanzania Digital

Kituo cha Uwekezaji Tanzania(TIC) kimewashauri Watanzania wameshauriwa kuendelea kuwekeza nchini ili kuongeza pato la Taifa.

Akizungumza na Waandishi wa Habari katika maonyesho ya 46 ya Kimataifa ya Biashara maarufu kama Sabasaba Afisa Forodha wa Kituo cha Uwekezaji(TIC), Leonard Mapunda amesema Serikali inaendelea kufanyia kazi malalamiko yanayotolewa na wawekezaji wa nje na ndani ya nchi katika maeneo ya Kisheria na Sera za kikodi ambapo yamekuwa yakilalamikiwa kwa kiasi kikubwa.

“Malalamiko hayo yanakuja kutokana na kubadilishwa kwa sheria za kikodi kila mwaka wa fedha hali inayowapelekea wawekezaji kushindwa kujipangilia vizuri majukumu yao,” amesema Mapunda.

Amefafanua kuwa TIC inaendelea kusaidia wawekezaji katika kuhakikisha wanaunganishwa na watu katika maeneo ya kuwekeza na mazingira rafiki kwao.

“TIC inatoa elimu kwa wawekezaji wa ndani na nje juu ya uwekezaji wa biashara katika sehemu mbalimbali nchini ikiwemo katika viwanja vya sabasaba,” amesema Mapunda.

Amesema elimu wanayoitoa ni pamoja na  ile ya sheria za kodi,sheria zao pamoja na vivutio vya uwekezaji.

Ameongeza kuwa Mwekezaji anapokuwa na cheti  hicho kinafanya kupeleka maombi kwa Kamishna wa Forodha ili kusudi aweze kusamehewa asilimi 75 ya kodi.

Ameongeza kuwa kazi kubwa ya Afisa Forodha ni kufatilia mchakato huo kwa Kamishna wa forodha mpaka hapo kibali kitakapotoka kwa Kamishina wa Forodha ili uwekezaji uendelee.

“Tunachowashauri wawekezaji watembelee ofisi zetu, Wizara ya Uwekezaji,Viwanda na Biashara watawapa elimu mbalimbali juu ya kupata taarifa pia kutembelea katika ofisi zetu za TIC ili kujifunza mengi juu ya uwekezaji,”amesema.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles