23.6 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Simba yaendelea kutoa vichapo

Na Winfrida Mtoi, Dar es Salaam

Timu ya Simba imeendelea kugawa dozi baada ya leo kushinda mechi yake ya kwanza ya Kombe la Mapinduzi kwa kuichapa Chipukizi mabao 3-1.

Katika mchezo huo uliopigwa katika Uwanja wa Amaan, Zanzibar, Chipukizi ilikuwa ya kwanza kupata bao dakika ya 36 kupitia Fakhi Mwalimu kabla ya Meddie Kagere kuisawazishia dakika ya 45.

Kipindi cha pili Simba ilirejea na kasi ambapo Miraji Athumani aliyeibuka mchezaji bora wa mechi baada ya kufunga mabao mawili yaliyokamilisha ushindi huo.

Wanamsimbazi hao ambao wamekwenda Zanzibar wakiwa na mzuka wa kupata ushindi mnono katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa kuifunga FC Platnum ya Zimbabwe mabao 4-0 na kutinga hatua ya makundi, kesho watashuka dimbani tena kuikabili Mtibwa Sugar.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles