30.2 C
Dar es Salaam
Tuesday, April 30, 2024

Contact us: [email protected]

Rais Samia kufanya ziara Uturuki

*Makamba asema itakuwa na manufaa kwa Tanzania

Na Esther Mnyika, Mtanzania Digital

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kufanya ziara nchini Uturuki kwa lengo la kukuza Uhusiano wa Kidiplomasia ya siasa, uchumi na biashara kati ya nchi hizo.

Akizungumza leo Aprili 15, jijini Dar es Salaam na waandishi wa habari Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, January Makamba amesema Rais Samia anafanya ziara hiyo kufuatia mwaliko alipewa na Rais wa Uturuki, Tayyip Erdogan.

Waziri Makamba amesema ziara hiyo itakayoanza Aprili 17 hadi 21, mwaka huu ni kubwa na ya kihistoria kwa Tanzania.

“Uturuki ni moja nchi ipo kwenye kundi la nchi 20 tajiri duniani (G20), hivyo tunajua ziara hiyo itakuwa ya kimkakakti. Lengo lingine ni kupata mtaji na teknolojia ambao nchi ya Uturuki wanayo, kupata masoko ya bidhaa ambayo yapo nchini humo na kushawishi wawekezaji kuja kuwekeza nchini kwetu,” amesema Mamkamba.

Amesema tayari wameshuhudia kampuni kubwa kutoka Uturuki zikifanya shughuli mbalimbali hapa nchini hatua ambayo imekuwa ikisaidia kuchochea maendeleo katika sekta mbalimbali zikiwamo za elimu, afya na maji.

Makamba amesema Rais Dk. Samia atafanya mazungumzo ya Kiserikali na Rais wa Uturuki na baadae watafanya mazungumzo ya pamoja na wajumbe wa pande zote mbili lengo likiwa ni kuangalia maeneo mapya ya ushirikiano.

Amesema miaka 14 iliyopita Rais aliyekuwepo madarakani alifanya ziara nchini humo na Rais wa Uturuki alikuja nchini mwaka 2017 hivyo kuna uhusiano wa muda mrefu kati ya nchi hizo mbili.

“Tuna uhusiano wa muda mrefu wa kidiplomasia tangu mwaka 1963 huku tukiwa tumefungua Ubalozi wetu mwaka 1979, baadae ubalozi huo ulifungwa mwaka 1984 kutokana na changamoto mbalimbali, ulifunguliwa tena mwaka 2009.

“Sisi tulikuwa na ubalozi nchini Uturuki uliofunguliwa mwaka 2017 hapo utaona kuwa uhusiano wetu ni mzuri kwa muda mrefu,” amesema Waziri Makamba.

Amesema Nchi ya Uturuki imekuwa haraka kiuchumi na ni nchi iliyopata maendeleo haraka kutokana na uhusiano na nchi za Afrika ikiwemo Tanzania.

“Tunajua kuna wafanyabiashara wengi wanakwenda Uturuki kununua bidhaa na sisi tunauza huko bidhaa zetu,” amesema Waziri Makamba.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles