23.6 C
Dar es Salaam
Thursday, May 9, 2024

Contact us: [email protected]

Rais Samia ateta jambo na Rais wa Brazil

Na Mwandishi Wetu, Mtanzania Digital

Rais Samia Suluhu Hassan akibadilishana mawazo na Rais wa Brazil, Lula Da Silva mara baada ya kukamilika kwa mkutano wa 15 wa Jumuiya ya BRICS.

BRICS ni Jumuiya kubwa ya pili ya kiuchumi duniani, ikiwakilisha idadi ya watu wanaokaribia bilioni 3.5. Jumuiya hii inaundwa na nchi 5 waanzilishi ambazo ni Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini.

Mkutano huu umetangaza rasmi nchi nyingine 6 zitajiunga na kuwa wanachama rasmi wa jumuiya hii kuanzia Januari 2024. Nchi hizo ni Argentina, Saudi Arabia, Egypt, UAE, Iran na Ethiopia.

Mahusiano mazuri kati ya Tanzania na Jumuiya hii inayokua kwa kasi yanaiongezea Tanzania wigo wa ushirikiano na fursa za kiuchumi.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
587,000SubscribersSubscribe

Latest Articles