23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

Oksijeni yaua wagonjwa wa corona

Nashik, India

Wagonjwa wa Corona 22 waliokuwa wamelazwa hospitali nchini India wamepoteza maisha kwa ukosefu wa Oksijeni kulikotokana na kuvuja kwa gesi hiyo.

Tukio hilo lilitokea jana katika Hospitali ya Zakir Hussain iliyoko jijini Nashik, wakati gari la Oksijeni likijaza hewa hiyo kwenye tanki la akiba.

Hata hivyo, bado haijafahamika kilichosababisha hewa hiyo kuvuja na kushindwa kuwafikia wagonjwa waliokuwapo hospitalini hapo.

Lakini maafisa walisema hapakuwa na oksijeni kwenye mashine za kusaidia kupumua kwa takriban dakika 30, na hivyo kusababisha vifo vya wagonjwa.

“Tutataka kuchunguza suala hili na kuchua hatua,” Kamishna wa manispaa ya jiji Kailash Jadhav alisema.

Hospitali kote nchini India zinahangaika kuendelea kuwapatia wagonjwa oksijeni huku wanaoihitaji wakiendelea kuongezeka.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles