27.5 C
Dar es Salaam
Thursday, April 25, 2024

Contact us: [email protected]

Watu wasiojulikana wavamia chuo, wateka Wanafunzi Nigeria

Abuja, Nigeria

Watu wenye silaha wameteka nyara wanafunzi kadhaa kutoka katika chuo kikuu kilichopo katika jimbo la Kaduna kaskazini mwa Nigeria.

Msemaji wa polisi katika jimbo hilo, Muhammad Jalige, amethibitisha utekaji nyara huo kwa BBC, akisema wanafunzi‘’wengi ‘’ wametekwa kutoka katika mabweni yao.

Lakini amesema shughuli ya kuhesabu wanafunzi bado inaendelaili kubaini idadi kamili ya wanafunzi waliotekwa. Waliotekwa ni wanafunzi wa kike na wakiume, aliongeza.

Watu wliokuwa wamebeba silaha walivamia Chuo Kikuu cha Greenfield kilichopo viungani mwa mki wa Kaduna Jumanne na kufyatua risasi.

Utekaji nyara kwa ajili ya kikombozi unaofanywa na watu wenye silaha umekuwa ukiongezeka katika miezi ya hivi karibuni nchini Nigeria, huku zaidi ya wanafunzi 800 wakiripotiwa kutekwa nyara mwezi wa Disemba.

Wengi wao wamekuwa wakiachiliwa baada ya mashauriano na watekajilakini wanafunzi 29 waliotekwa mwezi uliopita kutoka katika chuo kilichopo katika eneo la msitu bado wanashikiliwa

Waalimu pia wamekuwa wakilengwa na mashambulio.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles