23.3 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Natural Bond Ent waanza na Buffalo Souljah

Christopher Msekena

KAMPUNI kubwa ya muziki kutoka Jamaica, Natural Bond Entertainment, wameweka wazi mpango wa kukuza muziki wa Afrika kwa kuanza kushiriki kwenye albamu, Unity ya Buffalo Souljah, staa wa muziki Afrika Kusini mwenye asili ya Zimbabwe.

Prodyuza wa lebo hiyo Jarome Elvie, ameliambia MTANZANIA kuwa katika albamu ya Buffalo Souljah yenye jumla ya nyimbo 23, Natural Bond Entertainment wametengeneza ngoma mbili ambazo ni Family aliomshirikisha Starface na No Man Bigger Than God.

“Tumemchagua King wa African Dancehall, Buffalo Souljah ambaye pia anafanya Riddim na Reggae. Lengo la Natural Bond Entertainment ni kukuza muziki wa Afrika, tumeanza kufanya kazi kwenye albamu inayoitwa Unity ya Buffalo Souljah kwa kutengeneza nyimbo mbili ambazo tunaamini zitafanya vizuri pia mashabiki wanaweza kufuatilia kazi zetu kwenye Instagram tunatumia @naturalbondent,” alisema Elvie.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles