23.4 C
Dar es Salaam
Saturday, April 27, 2024

Contact us: [email protected]

King 98 afunguka alivyomnasa Diamond

Christopher Msekena

MSANII mwenye umri mdogo kutoka Zimbabwe, Ngonidzashe Dondo a.k.a King 98, amesema staa wa muziki nchini Nigeria, Davido, alimchongea njia ya kukutana na Diamond Platnumz mpaka wakafanikiwa kufanya kolabo yao, Kachiri.

Akizungumza na MTANZANIA hivi karibuni jijini Dar es Salaam, King 98 ambaye yupo Tanzania kwa ziara ya kimuziki, alisema licha ya ukubwa wa Diamond ni mtu mnyenyekevu aliyempa ushirikiano mwanzo mpaka mwisho.

“Nilikuwa nafanya vizuri Afrika Kusini na wimbo, Wacko niliofanya na Nasty C pia nimeshafanya ngoma na Davido inayoitwa No Bad Vibes. Davido ndio alipendezkeza nifanye ngoma na Diamond, tukawasiliana tukapanga namna ya kukutana tukafanya audio na video ya Kachiri.

 “Wakati tunafanya video ya Kachiri niligundua Diamond ni mtu ‘hambo’ sana, amenishika mkono na akaweka asilimia 100 ya nguvu zake kwenye kazi yangu, naweza kusema ilikuwa rahisi kufanya naye kazi,” alisema King 98.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles