BONN: Ujerumani
MHAMIAJI kutoka Syria aliyekataliwa kupewa hifadhi Ujerumani mwaka jana, amejilipua ndani ya baa na kuwajeruhi wa 12, watatu kati yao wakiwa katika hali mbaya.
Taarifa zinasema mtuhumiwa wa shambulio la kujitoa mhanga, anadhaniwa kuwa na uhusiano na mtandao wa ugaidi wa ISIS na alikuwa akisubiriwa kurudishwa Bulgaria.
Mtuhumiwa huyo ( 27), alijilipua katika mji wa Ansbach saa 4.00 usiku katika tamasha la muziki lililokuwa na watazamaji zaidi ya 2,500 ambao waliondolewa na kusimamishwa tamasha hilo ili kuimarisha ulinzi.
Hilo ni shambulio la tatu Bavaria katika kipindi cha wiki moja.
Ijumaa iliyopita, watu tisa waliuawa katika shambulio la ufyatuaji risasi mjini Munich lililofanywa na kijana Ali Sonboly (18).
Kabla ya hapo, kijana mwingine aliwashambulia watu kwa kisu na shoka katika treni.