24.1 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Mhagama ataka ujenzi vituo 20 kupima Ukimwi uharakishwe

FRANCIS  GODWIN, IRINGA

WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya  Waziri Mkuu (Sera  ,Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Watu  wenye  Ulemavu, Jenista Mhagama  ameagiza  ujenzi  wa  vituo  20 vitakavyotoa  huduma  za ugonjwa   Ukimwi kwa   wasafiri wa  masafa marefu vinavyojengwa chini ya Programu  ya Sattf   barabara kuu ya Dar es Salaam  kwenda nchi za  kusini mwa Tanzania kukamilisha ujenzi  huo ndani ya  mwezi mmoja.

Alitoa  agizo  hilo juzi,baada ya kuwekaji wa jiwe la msingi  kituo cha afya  Ipogolo  mjini  Iringa  kwa niaba ya  vituo  vingine.

Alisema hajafurahishwa na kasi  ndogo ya  ujenzi wa vituo  hivyo  ambavyo  kimsingi ujenzi  wake  ulipaswa  kukamilika tangu  Oktoba, mwaka huu.

Alisema  ujenzi  wa  vituo   20  kutoka  Dar es Salaam  hadi  Tunduma – Momba mpakani  wa Tanzania na  Zambia,Serikali  imekwishatumia  Dola za  Marekani milioni 3,  japo  kasi ya ujenzi  inasuasua.

Alisema  kutokana na  kasi ya Serikali uboreshaji wa  huduma  za  afya   ujenzi wa vituo  hivyo  utasaidia   kupunguza kasi ya maambukii ya  virusi vya ugonjwa huo kwa  wasafiri   wanaotumia barabara  hizo.

Alisema kupitia   fedha  hizo pamoja na kukamilisha ujenzi  wa vituo, pia  zitawezesha  kununua vifaa vya  kisasa na kuweka mazingira  wezeshi ya  kufundisha  wataalamu 10 kila  kituo watapata mafunzo.

Alisema lengo la kuwafundisha  wataalamu hao,  ni  kuondoa  usumbufu  wa  uhaba wa wahudumu katika vituo ili  wateja  watakapofika wapate huduma kwa wakati.

Alimtaka   Mkurugenzi  Mkuu wa  Tume ya Kuthibiti Ukimwi Tanzania (TACAIDS )  kuangalia  uwezekano wa kuanzisha mpango wa ujenzi wa  vituo kama  hivyo maeneo ya mipakani.

Alisema  ili  vituo  lazima  viweze endelevu na  kutoa  huduma  zake  kwa kipindi  kirefu zaidi ni  vizuri suala la  utunzaji  na usimamiazi wa miundombinu.

Katika  hatua  nyingine,Waziri Mhagama  aliahidi  kuanzisha  ujenzi  wa chumba  cha upasuaji na chumba  cha uzazi  kituo cha afya Ipogolo  na yeye atachangia  mifuko 100 ya saruji na bati 100 kama  sehemu ya  kuunga mkono.

” Ninalazimika  kuchangia bati  na saruji  ili  kuanza  ujenzi  wa  chumba cha upasuaji na chumba  cha uzazi,  nimefurahi  kukutana na Rosemary  Mwenda  ambae  leo amepata mtoto  katika  kituo hiki tena mtoto wa  kike  ambae  nimempa jina la Jenista,mimi ni mama  yake wa hiari baada ya mzazi wake  kufikisha ombi la kujengewa  vyumba,”alisema.

Kuhusu    kasi ya mambukizi ya virusi wa  vya  Ukimwi (VVU) mikoa ya  Njombe , Iringa na Mbeya, Mhagama  alisema   inatisha  na kuna haja ya  mikoa hiyo  kuweka mkakati wa  kupunguza kasi hiyo.

Mkuu wa  Wilaya ya Iringa, Richard Kasesela alisema  mkoa huo umepatiwa  vituo vinne   Wilaya ya Kilolo,kimoja  na  Iringa  vituo  vitatu ambavyo  vitasaidia  kupunguza kasi ya maambukizi.

Mkurugenzi  Mtendaji wa TACAIDS,Dk. Leonard Maboko  alisema  Tanzania ni miongoni mwa  nchi  za   kusini  mwa Jangwa la  Sahara  ambazo zinakabiliwa na kiwango kikubwa  na tatizo la ugonjwa huo,huku takwimu  zikionyesha  watu takribani milioni 37.9 wanaishi na maambukizi ya  VVU mwishoni  mwaka 2018 duniani , kati ya hao asilimia   53 wapo nchi  za  mashariki na kusini  mwa Afrika .

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles