25.2 C
Dar es Salaam
Friday, April 26, 2024

Contact us: [email protected]

Meek Mill atarajia mtoto

New York, Marekani

RAPA Meek Mill, ambaye alikuwa mpenzi wa staa wa muziki huo Nicki Minaj, amethibitisha kuwa anatarajia mtoto wa kwanza na mpenzi wake wa sasa Milan Harris.

Meek Mill aliwahi kuwa kwenye uhusiano na rapa Nicki Minaj, lakini wakaachana mwaka mmoja uliopita na wiki iliyopita wawili hao waliingia kwenye mgogoro katika mitandao ya kijamii wakitupiana maneno machafu.

Jana msanii huyo alitumia ukurasa wake wa Instagram kuweka wazi kuwa anatarajia mtoto wake wa kwanza na mpenzo wake Milan. Hivyo mashabiki wanaamini mgogoro wake na Nicki Minaj ulikuwa kwa ajili ya kutaka kuipa nguvu taarifa ya kutarajia mtoto.

“Ninayo furaha kwamba mpenzi wangu ana ujauzito, hivyo tunatarajia kupata mtoto mwaka huu ni jambo la furaha,” aliandika msanii huyo.

- Advertisement -

Related Articles

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here

Stay Connected

90,904FansLike
214,997FollowersFollow
586,000SubscribersSubscribe

Latest Articles